HUDUMA YA REDIO SAFINA KESHO IMEANDAA MAOMBI MAALUM YA KUKAA MBELE ZA MUNGU KWA MUDA MREFU ILI KUOMBA TOBA NA REHEMA JUU YA VITENDO VIOVU.


ARUSHA

Imebainishwa kuwa maadili ya mtu,jamii, au taifa yanapo poromoka shetani hupata mwanya wa kuingiza roho chafu inayomfanya Mungu kuachilia adhabu juu ya watu yakiwemo majanga ya njaa na magonjwa.

majanga ya njaa.
majanga ya njaa.




Huduma ya redio safina jijini Arusha kesho kwanzia saa mbili asubuhi hadi saa sita mchana imeandaa maombi maalumu ya kukaa mbele za Mungu kwa muda mrefu kwa ajili ya kuomba toba na rehema juu ya vitendo viovu kama vile unyanyasaji wa kijinsia,wanandoa kuingiliana kinyume na maumbile pamoja na ndoa za jinsia moja yaani ushoga.

Aidha kutokana na kuporomoka kwa maadili kwa baadi ya watu katika jamii kumetajwa kuwa chukizo mbele za Mungu na chanzo cha mateso na kilio katika familia ikiwemo ndoa kuvunjika,kuzidi kwa magojwa ya zinaa,uchumi kuporomoka kutokana na ghadhabu ya Mungu kuharibu vyanzo vyote vya uchumi kwa wote wanaoasi sheria na amri zake.

Pia kutokana na laana inayopiga  uchumi baada ya kuporomoka kwa maadili kwa kuwepo na ndoa za jinsia moja ukatili na unyanyasaji kwa wanandoa kesho katika ukumbi wa maombi uliopo mbauda jijini Arusha kutafanyika maombi ya toba na rehema kumuomba Mungu aondoe roho chafu ndani ya jamii na kukomboa uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.



HUDUMA YA REDIO SAFINA KESHO IMEANDAA MAOMBI MAALUM YA KUKAA MBELE ZA MUNGU KWA MUDA MREFU ILI KUOMBA TOBA NA REHEMA JUU YA VITENDO VIOVU. HUDUMA YA REDIO SAFINA KESHO IMEANDAA MAOMBI MAALUM YA KUKAA MBELE ZA MUNGU KWA MUDA MREFU ILI KUOMBA TOBA NA REHEMA JUU YA VITENDO VIOVU. Reviewed by safina radio on March 07, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.