WANAWAKE EAC WAUNGANA NA WANAWAKE WAOTE DUANIA KUADHIMISHA SIKUKUU YAO.
ARUSHA.
Wanawake wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC)
wameungana na wanawake wote duniani kuadhimisha siku ya wanawake kwa kutoa
vifaa Tiba katika hosipitali ya mkoa wa Arusha Mt Meru.
Akikabidhi vifaa hivyo Naibu Katibu mkuu wa
Jumuiya hiyo,Jescah Eriyo amesema kuwa anatambua moyo wa kina mama katika
kuifanya kazi hivyo ambapo amewataka kuendelea kufanya kazi kwa moyo wa
kujitoa na kutambua kuwa mwanamke ana nafasi kubwa katika jamii.
Akitoa shukrani kwa niaba ya wafanyakazi wa
hospitali hiyo mganga mfawidhi Dr Jackline Urio ameishukuru jumuiya hiyo
kwa kuona umuhimu wa kutoa vifaa Tiba katika hospitali hiyo kwani ni
jambo lenye tija katika jamii .
Hata hivyo miongoni mwa vifaa vilivyotolewa ni pamoja
na mashuka huku vifaa tiba vyenye thamani ya dola elfu nne vikitarajiwa
kukabidhiwa hivi karibuni katika hosipitali hiyo na Jumuiya hiyo.
Naye Naibu Meya wa Jiji la Arusha Viola
Likindikoki amesema kuwa changamoto za wanawake bado zinatajwa hususani maeneo
ya vijijini ikiwemo ukeketaji wa watoto wa kike kwa baadhi ya jamii,
mwanamke kunyanyaswa pindi anapotafuta ajira pamoja na wengine kutopata haki
zao.
WANAWAKE EAC WAUNGANA NA WANAWAKE WAOTE DUANIA KUADHIMISHA SIKUKUU YAO.
Reviewed by safina radio
on
March 08, 2018
Rating:

No comments