MNYETI AAHIDI KUWAPELEKA WATAALAMU WA ARDHI KUTOKA DODOMA KWENDA MANYARA .


MANYARA.

Mkuu wa Mkoa wa Manyara Bw Alexsander Mnyeti ameahidi kuwaleta wataalamu wa Ardhi kutoka Mkoani Dodoma ili kumaliza mgogoro wa ardhi ulioleta mtafaruku dhidi ya wananchi wa Kijiji cha Kimotorok Wilayani Simanjiro na Pori tengefu la Mkungunero.

Bw Alexsander Mnyeti.

Akizungumza Wilayani Simanjiro katika Ziara yake ya siku moja Bw Mnyeti ametembelea na kukagua eneo hilo ambalo limekuwa likilalamikiwa na wananchi kwa muda mrefu na kuahidi kuleta wataalamu ambao watabainisha mipaka halisi ya eneo hilo.

Mkuu huyo wa Mkoa amewataka wakuu wa mamlaka ya hifadhi kuacha kujiwekea mipaka kiholela bila kuwashirikisha wananachi na halshashauri badala yake kazi hiyo ifanywe na Halmashauri kwa kuwa inamamlaka isiyoegemea upande wowote.

Pia amesema kuwa ili kumaliza migogoro baina ya hifadhi na wananchi,wataomba mipaka ibadilishwe ili kuwaachia nafasi wananchi waliokuwa wakiishi kwa muda mrefu katika eneo hilo.

Aidha baadhi ya Wananchi wa eneo hilo  wamesema kuwa zoezi hilo la kusogezwa kwa mipaka ya hifadhi kwenye maeneo yao yalianza mwaka 2004  ambapo awali mpaka wao ulikuwa mwisho wa uwanja wa ndege ambao ulichongwa miaka ya 1980 na wananchi.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro Zephania Chaula kuhakikisha kuwa ndani ya siku nne anatatua mgogoro wa viongozi wa serikali ya kijiji cha Narokauwo ambao umewasababisha wananchi kuikataa serikali hiyo.




MNYETI AAHIDI KUWAPELEKA WATAALAMU WA ARDHI KUTOKA DODOMA KWENDA MANYARA . MNYETI AAHIDI KUWAPELEKA WATAALAMU WA ARDHI KUTOKA DODOMA  KWENDA MANYARA . Reviewed by safina radio on March 08, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.