MKUU WA WILAYA YA MONDULI BW. KIMANTA AZITAKA HALMASHAURI NA WADAU KUTENGA MAENEO YA UJENZI WA VIWANDA VIPYA.


ARUSHA.

Mkuu wa Wilaya ya Monduli Bw. Idd Hassan Kimanta amezitaka Halmashauri zote pamoja na wadau kuhakikisha wanatenga maeneo ya ujenzi wa viwanda vipya ili kuweza kuwavutia wawekezaji sambamba na kujenga uchumi wa kati.

Kimanta ameyasema hayo wakati akifungua Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Mrisho Gambo kikao kilicholenga kupitia na kuidhinisha mipangp ya bajeti ya sekretariet ya Mkoa na halmashauri zote kwa mwaka ujao wa fedha 2018/19.

Kimanta amesema kuwa bajeti hiyo ambayo ilijadiliwa katika ngazi ya Mkoa na kuwasilishwa kwa wajumbe imeonesha mafanikio kwa mwaka wa bajeti wa 2017/18 pamoja na changamoto zinazopaswa kuboreshwa katika kipindi cha mwaka wa fedha ujao.

Ameongeza kwa kusisitiza halmashauri kuendelea kusimamia zoezi la ukusanyaji wa mapato ya ndani kwani mwezi februari 2018 walikusanya mapato ya ndani kwa asilimia 57 huku wakitakiwa kukusanya  mapato kwa asilimia 100 ifikapo mwishoni mwa mwezi June mwaka huu.

Pamoja na hayo amezitaka halmashauri zijikite katika kukamilisha miradi ya maendeleo yenye kuleta tija kwa wananchi badala ya kuwa na miradi mingi ambayo haina tija na viongozi wa serikali kuwahimiza wananchi kujishughulisha na sekta za ufugaji,kilimo,utalii,viwanda na biashara ili kujiinua kiuchumi.

MKUU WA WILAYA YA MONDULI BW. KIMANTA AZITAKA HALMASHAURI NA WADAU KUTENGA MAENEO YA UJENZI WA VIWANDA VIPYA. MKUU WA WILAYA YA MONDULI BW. KIMANTA AZITAKA HALMASHAURI NA WADAU KUTENGA MAENEO YA UJENZI WA VIWANDA VIPYA. Reviewed by safina radio on March 08, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.