KIHAMIA AWAOMBA WAFADHILI KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KATIKA KUTATUA CHANGAMOTO ZINAZOIKABILI TAASISI ZA KIELIMU.
ARUSHA.
Mkurugenzi
wa Jiji la Arusha Bw Athuman Kihamia amewaomba wafadhili mbalimbali
kushirikiana na serikali katika kutatua changamoto mbalimbali zinazokabili
baadhi ya shule za msingi hapa nchini ikiwemo miundombinu ya vyoo na madarasa.
![]() |
Mkurugenzi wa Jiji la Arusha Bw Athuman Kihamia. |
Amesema
kuwa kwa sasa wana uhitaji mkubwa wa matundu ya vyoo kwenye shule za msingi
katika jiji la Arusha hivyo amemuomba mfadhili huo kuendelea na upendo wake wa
kutatua changamoto hizo kwa kuwashirikisha marafiki na kumwahidi kuwa serikali itanedelea
kushirikiana nae kwa juhudi zake za kuchangia maendeleo.
Kwa
wake bi Isabela Mwampamba ambaye pia ni mmiliki wa shule ya upendo friends amesema
kuwa aliamua kujitolea kama mfadhili wa ndani kwa kuwashirikisha marafiki mbali
mbali ili kuwezesha kutatua changamoto ya vyoo vya kisasa ambavyo wanafunzi
hao wenye ulemavu wa macho walikuwa wakikabiliwa nayo.
Hata
hivyo mradi huo wa vyoo wenye matundu sita umegharimu zaidi ya shilingi milioni
22 hadi kukamilika kwake.
KIHAMIA AWAOMBA WAFADHILI KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KATIKA KUTATUA CHANGAMOTO ZINAZOIKABILI TAASISI ZA KIELIMU.
Reviewed by safina radio
on
March 09, 2018
Rating:

No comments