WAKULIMA SIMANJIRO WASHAURIWA KUTUMIA MBOLEA YA KUPANDIA KATIKA MSIMU HUU WA KILIMO ILI KUVUNA MAZAO MENGI.


MANYARA.

Wakulima wa wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara wametakiwa kutumia mbolea za kupandia mazao katika msimu huu wa kilimo ili waweze kuvuna mazao mengi na kukuza uchumi wao na kuondokana na umaskini.


Wito huo umetolewa na Afisa Mazao wa halmashauri ya wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara Bw Erick Shoo wakati akizungumza na Redio Safina kuhusiana na matumizi bora ya mbolea katika msimu huu wa kilimo wilayani humo.

Amesema kuwa wakulima wengi wa wilaya hiyo hawana utaratibu wa kutumia mbolea katika kilimo chao kwa madai kuwa ardhi yao ina rutuba ya kutosha jambo ambalo linawasababishia kuvuna mazao machache na kuambulia kupata hasara tofauti na matarajio yao.

Aidha Bw Shoo ameongeza kuwa wanaendelea kushirikiana na watalamu kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa matumizi bora ya mbolea,ambapo baadhi ya wakulima waliotumia mbolea kwa msimu uliopita wamepata mafanikio makubwa katika kilimo chao tofauti na wale wanaofanya kilimo cha mazoea.

Naye mmoja wa mkulima wa halmashauri hiyo kutoka kijiji cha Langai Bw Daniel Andrea amesema kuwa kinachowafanya wasitumie mbolea katika kilimo chao ni kutokana na ardhi ya Simanjiro kuwa na rutuba ya kutosha hivyo wanahofia kuwa kutumia mbolea kunaweza kuwaharibia ardhi yao.

Hata hivyo msimu wa kilimo katika wilaya ya Simanjiro huanza mwanzoni mwa mwezi March kwa wakulima kuanza kuandaa mashamba kwa kusafisha kwa kutumia nyenzo mbalimbali ikiwemo Trekta.

WAKULIMA SIMANJIRO WASHAURIWA KUTUMIA MBOLEA YA KUPANDIA KATIKA MSIMU HUU WA KILIMO ILI KUVUNA MAZAO MENGI. WAKULIMA SIMANJIRO WASHAURIWA KUTUMIA MBOLEA YA KUPANDIA KATIKA MSIMU HUU WA KILIMO ILI KUVUNA MAZAO MENGI. Reviewed by safina radio on March 09, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.