URUSI YAPENDEKEZA MKUTANO WA USO KWA USO KWA MAWAZIRI WA MAMBO YA NJE WA PANDE ZOTE.


MOSCOW.

Urusi imependekeza kuandaliwe mkutano wa ana kwa ana kati ya Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Urusi Sergei Lavrov na mwenzake wa Marekani Rex Tillerson wakati mawaziri hao wote wakiwa ziarani barani  Afrika.

Moscow.
Naibu Waziri wa Mambo ya nchi za nje wa Urusi Sergei Ryabkov amesema masuala yanayostahili kujadiliwa yanaongezeka, ndio maana wametoa pendekezo hilo.

Lavrov na Tillerson watazuru Ethiopia wiki hii lakini Ryabkov amesema hawana taarifa yoyote kuhusu kama ratiba zao huenda zikaunganishwa.
Lavrov alianzia ziara yake ya siku tano barani Afrika jana Jumatatu nchini Angola na anapanga kuzitembelea Namibia, Msumbiji, Zimbabwe na Ethiopia ambapo atakuwa katika mji mkuu Addis Ababa mnamo Machi 8 na 9.

Kwa upande wake Tillerson atazuru nchi za Kiafrika ikiwemo Ethiopia kati ya Machi 6 na 13 kwa mujibu wa msemaji wa wizara ya mambo ya nje.


URUSI YAPENDEKEZA MKUTANO WA USO KWA USO KWA MAWAZIRI WA MAMBO YA NJE WA PANDE ZOTE. URUSI YAPENDEKEZA MKUTANO WA USO KWA USO KWA  MAWAZIRI WA MAMBO YA NJE WA PANDE ZOTE. Reviewed by safina radio on March 06, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.