ZAIDI YA TANI 100 ZA TAKA HUZALISHWA KWA SIKU KATIKA MJI WA TUNDUMA MKOANI SONGWE.


SONGWE.

Wakazi wa Mji wa Tunduma mkoani Songwe wameanza kukumbwa na hofu ya kupata magonjwa ya mlipuko kutokana na ongezeko kubwa La taka zinazozalishwa katika mji huo ambapo kwa siku halmashauri ya mji huo huzalisha tani 150 za taka.

Mrundikano wa taka.
Hayo yabebainika wakati wa mkutano kati ya wakazi hao na Mkuu wa Wilaya ya Momba Juma Said Rando uliofanyika katika mji wa Tunduma wametoa kero yao kwa mkuu huyo,ambapo Mkuu huyo wa Wilaya ameonyesha kukerwa na suala hilo la mrundikano wa taka katika mji huo wa Tunduma.

Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Fedha katika halmashauri ya mji wa Tunduma Bw. Onesmo Moga kwa niaba ya Bwana Afya amekiri kuwa mji wa Tunduma ni mji wenye changamoto ya mrundikano wa Taka kutokana na Mji huo kutokuwa namiundombinu rafiki na isiyopitika kwa urahisi.

Hata hivyo Bw. Moga amewahakikishia wananchi kumaliza kabisa tatizo hilo katika halmashauri ya mji huo ili kuepusha matatizo mengine yatakayoweza kutokea ya kiafya.

ZAIDI YA TANI 100 ZA TAKA HUZALISHWA KWA SIKU KATIKA MJI WA TUNDUMA MKOANI SONGWE. ZAIDI YA TANI 100 ZA TAKA HUZALISHWA KWA SIKU KATIKA MJI WA TUNDUMA MKOANI SONGWE. Reviewed by safina radio on March 06, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.