MIKOA YA KASKAZINI MWA TANZANIA YA ATHIRIKA ZAIDI KWA UGONJWA WA FIGO.


DAR-ES-SALAAM.

Utafiti umebaini kuwa kila watu kumi mmoja anatatizo la figo huku mikoa ya Kaskazini mwa Tanzania ikionekana kuwa asilimia saba ya wananchi waliofanyiwa utafiti katika maeneo yao wanatatizo la ugonjwa wa figo hali inayoonyesha tatizo hilo kuwa kubwa nchini.

figo lililoshambuliwa na magonjwa.
Hayo yamebainishwa leo na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Figo kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam Dk. Onesmo Kisanga ambapo amesema kuwa kina mama wengi ni waathirika wakubwa wa tatizo hilo la figo kuliko wanaume kutokana na uzazi.

Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Figo, Onesmo Kisanga wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) LEO akizungumzia kuhusu umuhimu wa kupima afya mara kwa mara ili kuzuia uwezekano wa mtu kupata matatizo makubwa ya magonjwa ya figo.

Aidha, Dk. Kisanga amesema kuwa katka maadhimisho ya siku ya figo duniani ambayo huuadhimishwa kila alhamisi ya pili ya mwezi machi wamelenga zaidi kuwasaidia wakina mama hao kupata huduma kwa haraka zaidi ili kupunguza tatizo hilo.

Dk. Kisanga amesema kuwa wakina mama wengi wanakuwa na matatizo mengi wakati wa kujifungua kama kutokwa na damu nyingi, pamoja na kupata kifafa cha mimba hivyo matatizo hayo kuweza kupelekea kupata tatizo la figo.

Amesema kuwa ugonjwa waLupodonor umekuwa unawashambulia zaidi wanawake ambapo kati ya wanawake ishirini wenyye ugonjwa huo mwanaume mmoja ndiye aliyeathirika.

Hata hivyo, amebainisha kuwa kwa sasa wameanza kupandikiza figo nchini ambapo mwanzoni mwa mwezi Novemba mwaka jana madaktari walianza kupandikiza figo ya kwanza katika hospitali ya Muhimbili sambamba na kuwa serikali imenza kutunga sheria ya kudhibiti biashara ya figo ambayo itasaidia kuthibiti uuzwaji huo kwa kuwa anayeuza anamdhulumu anayeuuzia.

MIKOA YA KASKAZINI MWA TANZANIA YA ATHIRIKA ZAIDI KWA UGONJWA WA FIGO. MIKOA YA KASKAZINI MWA TANZANIA YA ATHIRIKA ZAIDI KWA UGONJWA WA FIGO. Reviewed by safina radio on March 06, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.