IMEBAINISHWA KUWA KUNA UWEZEKANO MKUBWA WA ADUI KUTUMIA MAJINA YA WATU VIBAYA KWA MAENEO AU VITENDO NA KUHARIBU MSINGI WA MAISHA IKIWEMO UCHUMI NA AFYA.


ARUSHA

Imebainishwa kuwa kuna uwezekano mkubwa wa adui kutumia majina ya watu vibaya kwa maneno au vitendo na kuharibu msingi wa maisha ikiwemo uchumi na afya.

ADUI KUTUMIA VIBAYA JINA.
Huduma ya redio safina kesho katika ukumbi wa maombi uliopo mbauda jijini Arusha kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa sita mchana imekuandalia maombi ya ukombozi wa jina la mtu na majina ya mahali anapoishi ili kudhibiti malango mabaya ambayo yamefunguliwa na adui kupitia jina.


Aidha kwa mujibu wa somo hilo wapo watu wengi ambao wanataabika kwa magonjwa sugu,umaskini,kufa kwa miradi,ndoa kuvunjika,pamoja na huduma,kutokana na baadhi ya majina ya watu hao kubeba roho ya mauti.

kufa kwa miradi.
Pia wapo wengine ambao majina yao yamepelekwa kwa wachawi na waganga wa kienyeji kwa lengo la kuondoa uhai au kurudisha nyuma maendeleo ya watu lakini imebainika kuwa damu ya Yesu Kristo ina uwezo wa kusafisha majina hayo na mtu kuwekwa huru.

Hata hivyo kesho mahitaji mbalimbali yataombewa katika ukumbi wa safina redio yakiwemo magonjwa,matatizo ya ajira,migogoro ya ndoa,pamoja kukomboa malango ya majina yaliyokuwa yakipitisha mauti au uchumi kuyumba.  

kukomboa malango ya majina.

IMEBAINISHWA KUWA KUNA UWEZEKANO MKUBWA WA ADUI KUTUMIA MAJINA YA WATU VIBAYA KWA MAENEO AU VITENDO NA KUHARIBU MSINGI WA MAISHA IKIWEMO UCHUMI NA AFYA. IMEBAINISHWA KUWA KUNA UWEZEKANO MKUBWA WA ADUI KUTUMIA MAJINA YA WATU VIBAYA KWA MAENEO AU VITENDO NA KUHARIBU MSINGI WA MAISHA IKIWEMO UCHUMI NA AFYA. Reviewed by safina radio on March 09, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.