RAIA 24 WAUAWA KUTOKANA NA MASHAMBULIZI MAKALI YA ANGA NA ARDHI, SYRIA.


DAMASCUS.

Mashambulizi makali ya angani na ardhini yanayoendelea kufanywa na jeshi la Syria katika eneo la Ghouta Mashariki, limewaua raia 24.



Shirika la haki za Binaadamu la Syria limethibitisha kuuawa na raia hao katika mashambulizi ya angani yaliyoendelea hapo jana.

Aidha habari zinaeleza kuwa jeshi hilo limekaribia kulikamata tena eneo hilo linalodhibitiwa na waasi huku wakisaidiwa na wanajeshi wa Urusi.

Msafara wa malori ya misaada ya Umoja wa Mataifa na Shirika la Msalaba Mwekundu uliotarajiwa kwenda katika eneo hilo jana, ulishindwa kutokana na mashambulizi makali yanayoendelea.

Zaidi ya raia 930 wameuawa katika mashambulizi hayo ya karibu wiki tatu kwenye ngome hiyo ya mwisho ya waasi nje ya mji mkuu Damascus, ambako watu kadhaa walishambuliwa na silaha za sumu.

RAIA 24 WAUAWA KUTOKANA NA MASHAMBULIZI MAKALI YA ANGA NA ARDHI, SYRIA. RAIA 24 WAUAWA KUTOKANA NA MASHAMBULIZI MAKALI YA ANGA NA ARDHI, SYRIA. Reviewed by safina radio on March 09, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.