WATU 16 WAFA KWA RADI NCHINI RWANDA.


TAREHE 12 MARCH 2018

media
Watu 16 waliouawa Jumamosi iliyopita baada ya kupigwa radi wakiwa katika Kanisa la Waadventista Wasabato katika Wilaya ya Nyaruguru nchini Rwanda wamezikwa.
Wauamini wote walizikwa katika Makaburi ya Nyabimata katika mazishi ambayo yalihudhuriwa na mamia ya waombolezaji.
Meya wa Wilaya ya Nyaruguru Habitegeko Francois ameliambia Shirika la Habari za Ufaransa AFP kuwa watu 14 walipoteza maisha  hapo hapo huku wengine wawili wakipoteza maisha wakiwa hospitalini.
Waumini wengine 140 walijeruhiwa kutokana na radi hiyo iliyoambatana na mvua kubwa na wanaendelea kupata matibabu katika hospitali mbalimbali katika Wilaya hiyo.
Mwanafunzi mmoja alipoteza maisha huku wengine 17 wakijeruhiwa katika tukio hilo baya la kiasili kuwahi kutokea Rwanda katika siku za hivi karibuni

WATU 16 WAFA KWA RADI NCHINI RWANDA. WATU 16 WAFA KWA RADI NCHINI RWANDA. Reviewed by safina radio on March 12, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.