MAAFISA 5 WA POLISI NCHINI AFGHANISTAN WAMEUAWA
TAREHE 13-03-2018
Afisa mmoja nchini
Afghanistan amesema kiasi ya maafisa watano wa polisi nchini humo wameuawa
baada ya waasi kushambulia eneo la ukaguzi katika jimbo la la magharibi la
Farah.
Hakuna mtu aliyedai
kuhusika na shambulizi hilo lakini kiongozi wa serikali kwenye jimbo hilo Fared
Bakhtawer anawahusisha wanamgambo wa Taliban na shambulizi hilo.
Mwishoni mwa wiki
wanamgambo wa Taliban waliwaua maafisa wa usalama 15 wa Afghanistan wakiwemo
makamanda wajeshi saba na maafisa wa polisi wanane katika wilaya ya Bala Bluki.
Haya yanajiri huku waziri wa ulinzi wa
Marekani Jim Mattis akiwasili katika mji mkuu wa Afghanistan Kabul katika ziara
ambayo haikutangazwa.
MAAFISA 5 WA POLISI NCHINI AFGHANISTAN WAMEUAWA
Reviewed by safina radio
on
March 13, 2018
Rating:
No comments