WAZIRI MKUU WA UINGEREZA THERESA MAY AMELIAMBIA BUNGE KUWA KUNA UWEZEKANO URUSI IMEHUSIKA KUMPA JASUSI SUMU
Waziri Mkuu wa
Uingereza Theresa May amewaeleza wabunge nchini humo kuwa kuna uwezekano Urusi imehusika na kumpa
sumu jasusi wazamani Sergei Skripal pamoja na binti yake katika mji wa kusini
wa Salisbury.
Waziri Mkuu Theresa May
Waziri Mkuu Theresa
May amesema iwapo ushahidi utathibitisha kuwa Urusi ilielekeza moja kwa moja
tukio hilo basi serikali ya Uingereza itachukulia kuwa ni shambulizi
lililofanywa kwa kutumia nguvu kinyume cha sheria katika ardhi ya Uingereza.
Katibu Mkuu wa NATO -
Jens Stoltenberg amesema tukio hilo linaibua wasiwasi mkubwa huku waziri wa
mambo ya nje wa Marekani Rex Tillerson akisema wana imani kubwa na uchunguzi unaofanywa
na Uingereza pamoja na tathimini yake kuwa huenda Urusi ikawa inahusika na
tukio hilo .
WAZIRI MKUU WA UINGEREZA THERESA MAY AMELIAMBIA BUNGE KUWA KUNA UWEZEKANO URUSI IMEHUSIKA KUMPA JASUSI SUMU
Reviewed by safina radio
on
March 13, 2018
Rating:
No comments