WANAFUNZI WAFANYA MAANDAMANO NCHINI TUNISIA
WANAFUNZI NCHINI TUNISIA. |
Wanafunzi wanaosomea taaluma ya udakitari nchini Tunisia
wamefanya maandamano nje ya ofisi ya Wizara ya Afya wakishinikiza kutekelezewa
matakwa yao.
Shirika la habari la AFP limeripoti kuwa, wanachuo na wanafunzi
wapatao 1,500 wameshiriki maandamano hayo katika mji mkuu Tunis, kuishinikiza
Wizara ya Afya kuheshimu haki na matakwa yao.
Hali kadhalika wameitaka serikali kuangalia upya mageuzi
yaliyopasishwa hivi karibuni na Wizara ya Afya, yanayotaka kurejeshwa nyuma kwa
miaka kadhaa utoaji wa cheti cha diploma kwa wanafunzi wanaosomea utabibu.
Maandamano haya yanajiri katika hali ambayo, Ofisi ya Rais
wa Tunisia mapema mwezi huu ilitangaza kwamba, muda wa hali ya hatari
umeongezwa nchini humo kwa miezi saba mingine.
Sheria ya hali ya hatari ilianza kutekelezwa nchini Tunisia
tarehe 24 Novemba 2015 baada ya kutokea shambulio la kigaidi dhidi ya basi moja
la askari wa ulinzi wa Rais mjini Tunis.
WANAFUNZI WAFANYA MAANDAMANO NCHINI TUNISIA
Reviewed by safina radio
on
March 13, 2018
Rating:
No comments