NAIBU WAZIRI NDITIE ASEMA KUWA SERIKALI INAENDELEZA KUTOA MAFUNZO YA TEHAMA.


Naibu Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano anayeshughulikia uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye amesema kuwa serikali inaendeleza juhudi za kutoa mafunzo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano-TEHAMA kwa walimu wa shule za umma ili kabiliana na tatizo la ukosefu wa ujuzi na upotevu wa fedha za serikali katika kuwalipa mafundi.

Naibu Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano anayeshughulikia uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye.
Naibu waziri Nditie ameyasema hayo mjini Dodoma wakati akifungua mafunzo ya TEHAMA kwa walimu wa Shule za Sekondari za umma nchini ambapo amesema kuwa ukosefu wa ujuzi wa TEHAMA umekuwa ukiisababishia serikali hasara.

Akitoa maelezo ya Mafunzo hayo kwa niaba ya Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Fursa sawa kwa wote MUKLAF, Katibu Mtendaji wa Mfuko huo Justina Mashiba amesema kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo walimu katika ufundishaji wa masomo ya TEHAMA.

Mafunzo hayo yametolewa kwa awamu ya pili baada ya kukamilika kwa awamu ya kwanza ambayo imeshirikisha waliu mia mbili themanini na sita.  

NAIBU WAZIRI NDITIE ASEMA KUWA SERIKALI INAENDELEZA KUTOA MAFUNZO YA TEHAMA. NAIBU WAZIRI NDITIE ASEMA KUWA SERIKALI INAENDELEZA KUTOA MAFUNZO YA TEHAMA. Reviewed by safina radio on March 13, 2018 Rating: 5

No comments