MKUU WA WILAYA YA GEITA HERMAN KAPUFI AMEPOKEA MAFUTA YA KUJIPAKA KWA AJILI YA WATOTO NJITI.



Mkuu wa Wilaya ya Geita Bw Herman Kapufi amepokea msaada wa mafuta ya kujipaka kwa ajili ya watoto njiti waliolazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita.

Mkuu wa Wilaya ya Geita Bw Herman Kapufi.
Bw. Kapufi amepokea msaada huo kutoka kwa Kituo cha kusaidia watoto Njiti cha Neya Pre-babies chini ya Mkurugenzi wake Happyness Mabula,ambapo ameshukuru kwa msaada huo wa mafuta.

Amesema kuwa msaada huo uliotolewa na Bi. Mabula si wa kutoa tumaini kwa watu wenye watoto hao pekee bali kwa yeye pia ambaye mtoto wake alizaliwa kabla ya wakati miaka mitatu iliyopita.

Kwa upande Muuguzi Kiongozi wa hospitali hiyo Charugamba Jackson amezungumzia changamoto ya hospitali hiyo kuwa na chumba kimoja cha kuhifadhia watoto njiti huku kikiwa na uwezo wa kuhifadhi watoto wanne pekee.

Aidha, amesema kuwa idadi ya watoto wanaozaliwa kabla ya wakati katika hospitali hiyo kwa mwezi ni watoto njiti thelathini wakati uwezo wake ni mdogo wa kuhifadhi watoto hao ambapo ameiomba jamii kujitokeza katika ujenzi wa wodi itakayokuwa na vyumba hivyo.

MKUU WA WILAYA YA GEITA HERMAN KAPUFI AMEPOKEA MAFUTA YA KUJIPAKA KWA AJILI YA WATOTO NJITI. MKUU WA WILAYA YA GEITA HERMAN KAPUFI  AMEPOKEA MAFUTA  YA KUJIPAKA KWA AJILI YA WATOTO NJITI. Reviewed by safina radio on March 12, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.